Home Music Ari Loveness Afunguka Sababu Ya Kuachia Nyimbo Mpya “Sitakata Tamaa”

Ari Loveness Afunguka Sababu Ya Kuachia Nyimbo Mpya “Sitakata Tamaa”


advertisement


Ari Loveness ni Binti anayekuja kwa kasi sana kutokea Mombasa Pwani ya Kenya, chini ya Lebo ya Neptune Records ya Producer maarufu Lameckboy Kenya the Young 001, Round hii ametisha kwa Kibao chake kipya cha Sitakata Tamaa, ambacho kimepikwa kikaiva ndani ya Neptune Records.

Hebu cheki alichokisema:;.

Mzuka Kibao: kwanini Uliimba Kibao sitakata tamaa?

Ari Loveness: Sitakata tamaa ni wimbo unaozungumzia hali halisi ya kile nachokipitia.

Mzuka Kibao: Unapitia nini hasa?

Ari Loveness: Kwakweli nimevunjwa moyo nlipoanza safari yangu ya mziki, nimedharauliwa sana, kufikia wakati waku give up.

Mzuka Kibao: Kipi hasa kwa sasa ambacho kimekupa morali nakupelekea we we kupata courage yakuendelea kuimba?

Ari Loveness: Support nayoipata kutokana na management yangu ya Neptune Records, ambayo producer wangu ananipea pia sapot from my familly na thamani ambayo mimi kama Msanii nafaa kupewa, imenishawishi pakubwa sana, nashukuru.

Mzuka Kibao: Je katika lebo ya Neptune Records, niwewe peke yako ambae umesainiwa ama mko wasanii wangapi na je huoni kutatizika labda wakati wakuachia kazi?

Ari Loveness: Neptune Records ipo na wasanii wengi ambao ata wengne hawajaskika Lakini muda wao ukifika mtawasikia, lakini kwa sasa wasanii ambao wanafanya vizuri tuko wanne (4), 1: Ari Loveness Mimi, 2: Allay Fabrizio, 3: Kaka Mswazi Kenya(Favoured Lamim),4:,Shy Man. Upande wakuachia kazi hainitatizi manake tuko na system yakuachia kazi yani tunakuwa twapishana.

Mzuka Kibao: Video ya sitakata tamaa inatoka lini?

Ari Loveness: Video tunaanza shooting Saturday 27 to Sunday 28 Oct 2018, kulingana na management. So mafans wakae wasubiri.

Mzuka Kibao: Asante kwa muda wako.

Ari Loveness. Asante pia na nashukuru.

Angalia picha za Ari Loveness

New Music | Ari Loveness – Sitakata Tamaa (Prod by Lameckboy Kenya)

DOWNLOAD MZUKA KIBAO NEW APP

FOR FAST LATEST UPDATES ON

AUDIOS, VIDEOS, MIXTAPES, FREE BEATS AND INSTRUMENTALS

CLICK HERE TO JOIN OUR WHATSAPP GROUP

Leave a Reply